Tuesday, November 22, 2011

Mashallaaaaah!Ng'ombe akichinjwa kwaajili ya kitoweo siku ya Eid Elhajj.Nyama iliandaliwa na wanajumuiya walifaidi pamoja na watoto yatima pia watu wa karibu walipata mgao ili nao washerehekee Eid Elhajj kwa furaha.
Nyama ikiandaliwa kwa waajili ya kuigawa kwa jumuiya ya watu wanaozunguka jumuiya ya chuo cha SAUT wakati wa sherehe ya Eid Elhajj mwaka 2011.Hakika ilikuwa siku ya furaha kubwa kwa wana SAMUCO.Mashallaaaaah.

Monday, November 21, 2011

Waislam wakisikiliza kwa umakini wa hali ya juu mada iliyokuwa ikwasilishwa katika ukumbi wa M1 katika chuo cha SAUT.
Mlezi pamoja na viongozi.Picha hii ilipigwa baada ya mahafali ya kuwaaga wahitimu wa mwaka 2010.
Sherehe na kumbukumbu.Wahitimu wamependeza.
Ustadh Hussein ambaye sasa anachukua masters akiwahutubia waislam katika ukumbi wa M11.
Mlezi wa SAMUCO Ndg.Altaf Hirani Mansoor akitoa hotuba kwa waislam chuo cha SAUT.
Amir wa TAMSYA mkoa Ndg.Ahmed Binde pamoja na naibu Amir wa TAMSYA Mkoa wa Mwanza Ndg.Abdul-Rasul Maheta wakimsindikiza mlezi Ndg.Altaf Hirani.

Amir wa TAMSYA akisoma risala ya wahitimu kwa mgeni rasmi.
Mlezi akimkabidhi katibu mhitimu zawadi.
Ndg.Altaf Hirani akiwa anapitia risala ya wahitimu kwa umakini mkubwa.
Mlezi wa SAMUCO akitoa msaada kwa mlezi mwakilishi wa kituo cha watoto yatima.
Mlezi wa SAMUCO akizungumza jambo na Rais wa TAMSYA katika mahafali iliyo fanyika chuo cha SAUT.
Rais wa TAMSYA akisikiliza linaloendelea katika ukumbi akiwa makini kabisa sambamba na mlezi wa SAMUCO katika mahafali ya kuwaaga wahitimu wa mwaka 2010 yaliyofanyika katika chuo cha SAUT kwenye ukumbi wa M11 mwaka2010.

Maamiri wastaafu kutoka SAUT na CBE wakisoma shairi katika mahafari ya kuwaaga wahitimu wa mwaka 2010.
Mlezi wa SAMUCO Ndg.Altaf Hirani akihojiwa na kituo cha ITV baada ya mahafali ya kuwaaga wahitimu wa Kiislam wa mwaka 2010 katika chuo cha SAUT.
Kina dada wa vyuo mbalimbali vya Mwanza wakiwa makini kusikiliza mada katika kongamano lililofanyika kaika ukumbi wa M1 chuo cha SAUT.

Friday, November 18, 2011


Katibu mkuu wa SAMUCO akitoa maelekezo wakati wa kugawa misaada kwa watoto yatima wa kituo cha Upendo Daima wakati wa mahafali2010.

Ndg.Altaf Hirani Mansoor akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu wa mwakajana 2010.

Mlezi wa SAMUCO Altaf Hirani akitafakari jambo wakati wa kongamano lililofanyika ukumbi wa M1 SAUT.

Wanajumuia wakiume wa SAUT wakiwa na makamu mkuu wa chuo kikuu cha SAUT Mwanza Rev. Dr.Charles Kitima na mlezi Altaf Hirani.

Rev.Dr.Kitima akiwa katika picha ya pamoja na wanawake wa jumuia ya samuco pamoja na mlezi wa samuco Altaf Hilani katika msikiti wa SAUT Mwanza

Tuesday, November 15, 2011

Dr.Kitima na mlezi wa SAMUCO Ndg.Altaf Hirani wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya vingozi.
Dr.Kitima vice chanceler wa saut akishirikiana na jumuiya ya SAMUCO kutoa misaada kwa yatima.
Mlezi Ndg.Altaf Hirani akipanda mti huku akitizamwa kwa karibu na katbu Bw.Abdulrasul Maheta.
Katibu wa SAMUCO Bw.Abdulrasul akikagua ujenzi wa upanuzi wa msikiti wa SAUT.
Katibu wa SAMUCO Bw.Abdu-rasul Maheta akitazama ujenzi wa sehemu ya kutawadhia katika msikiti wa SAUT.
Amiri wa SAMUCO Ndg.Makame Ally akipanda mti katika kuhifadhi mazingira.

Mlezi wa SAMUCO Ndg.Altaf Hirani akipiga picha ya pamoja na watoto yatima.
Mlezi wa SAMUCO Ndg.Altaf Hirani akitoa maelekezo kwa makatibu Abdul-rasul Maheta na Mbarouk Matata juu ya upanuzi wa msikiti na jumuiya ya SAMUCO.

MWANAFUNZI AJINYONGA CHUO CHA SAUT.

Mwanafunzi wa sheria mwaka wa kwanza katika chuo cha Mt.Augustine campus ya Mwanza amejinyonga hadi kufa.Mashuhuda wa tukio hilo lililotokea siku ya jumamosi tarehe 12/11/2011,wanasimulia kuwa walimkuta mwanafunzi huyo akiwa ananing'inia juu ya mti nyuma ya maktaba ya chuo.Histori ya mwanafunzi huyo mkimya wa sheria inasemekana tabia yake hiyo ya ukimya ndio iliyomponza.Kwani inaelezwa kuwa jamaa huyo kutoka Mkoa wa Kilimanjaro alikuwa hana muda wa kuzungumza na wenzake,hivyo wanafunzi wa karibu yake ambao analala nao chumba kimoja cha bweni walianza kumchokoza ili azungumze.Wakaamua kumtengenezea kashfa mbaya ya ushoga ambapo kila wakati walikuwa wakimwita shoga kitendo ambacho kilimuudhi marehemu.Habari za yeye kuwa shoga zilienea na kumfikia rafiki yake wa kike ambapo naye alimwambia ajijue kivyake kwani yeye hawezi kuwa na mwanaume wa namna hiyo.Kibaya zaidi ni kuwa watu wa karibu ndio walienda kwa binti huyo na kumwambia rafiki yake ni shoga.Lengo lao ilikuwa wamuudhi ili azungumze tu lakini ikashindikana na marehemu akafikia uamuzi mzito wa kujinyonga.Marehemu aliacha ujumbe wa sababu za yeye kujinyonga na kuwataja wote waliomtengenezea kashfa hiyo chafu.Mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda Kilimanjaro kwaajili ya maziko.Matukio ya kujinyonga chuo cha SAUT yamekuwa yakiripotiwa mara kadhaa.Innalillah Wa inna Ilayh Rajiuun.

Friday, November 11, 2011

WANAWAKE WASOMI WA KIISLAM KUFANYA KONGAMANO KUBWA KESHO.

Wanawake wa kiislam ambao ni wasomi kutoka vyuo vikuu jijini Mwanza kufanya kongamano kubwa katika ukumbi wa M3 uliopo Malimbe katika chuo kikuu cha Mt.Augustino-SAUT.Kongamano hilo litawakutanisha wasomi wanawake kutoka katika vyuo mbalimbali vya jiji la Mwanza.Mada zitakazo jadiliwa ni pamoja na Haki Ya Mwanamke Kwa Mumewe,Kupenda Ni Nini?Kwa Mtazamo wa Uislam na mengineyo yanayohusu Wanawake.Wahadhiri katika kongamano hilo ni Shekhat Zabibu kutoka Mwanza na wengine kutoka Mombasa,Kenya.Hivyo Waislam wote kinadada na kinamama mnakaribishwa sana.

Sunday, November 6, 2011

WAISLAM SAUT WAKISHEREHEKEA EID EL-HAJI.

Swala ya eid el-haji iliswaliwa kwenye msikiti wa chuo na kuswalishwa na Sheikh Hassan Kabeke ambaye ni maarufu jijini Mwanza.Kwakuwa eid el-haji ni eid ya kuchinja,hivyo Ng'ombe alichinjwa na nyama kugawiwa swadaka kwa jumuiya inayozunguka chuo cha St.Augustine.Pia jumuiya ya wanachuo wakiislam walishiriki na watoto yatima wa kituo cha Upendo Daima kilichopo Malimbe.Mbali ya kushiriki na watoto hao pia watoto hao walipewa vitu mbalimbali kama mafuta,sabuni,mchele na mbuzi mmoja.Vitu hivyo vilikabidhiwa na makamu mkuu wa chuo (vc)Father Charles Kitima.Jumuiya ya Waislam pia walisherehekea eid kwa kupanda miti mia moja na tatu,mitatu ikiwa ya matunda na mingine ya kawaida wakiongozwa na makamu mkuu wa chuo Dr.Kitime pamoja na mlezi mkuu wa jumuiya ya waislamu SAMUCO ndugu Altf Hirani.

Tuesday, November 1, 2011




Katika kongamano lililofanyika katika ukumbi wa M1 Jumapili ya tarehe 30/10 katika chuo cha Mt.Augustine(SAUT) cha jijini Mwanza.Kongamano lilikuwa maalum kwa kuwakaribisha mwaka wa kwanza,na kuwakutanisha wanafunzi wa vyuo vyote vya Mwanza. Vyuo vilivyoshiriki ni pamoja na wenyeji SAUT,CUHAS,BUTIMBA,FISHARIES,Ukiliguru,CBE,VETA na vyuo vingine jirani.Mashekh waliohudhuria kongamano hilo ni pamoja na Ust.Ilunga Kapungu(picha no2) pamoja na Ust.Hassan Kabeke(picha no3).Mashekhe wakiwaasa wasomi hao kwa ujumla kuacha kubadili tabia pindi wanapofika vyuoni na kuacha maadili ya Uislam.Kwani wengi wakifika vyuoni hawataki kujulikana kama wao ni waislam.Pia walitoa wito kwa wasomi mara wanapohimu kwenda kuzisaidia taasisi za kiislam badala ya kukaa pembeni na kulaum pindi mambo yanapokwenda kombo. Waislam pia wameaswa kuunganisha tabaka mbili zilizopo za walio na elimu ya mazingira na elimu ya dini.