Sunday, November 6, 2011

WAISLAM SAUT WAKISHEREHEKEA EID EL-HAJI.

Swala ya eid el-haji iliswaliwa kwenye msikiti wa chuo na kuswalishwa na Sheikh Hassan Kabeke ambaye ni maarufu jijini Mwanza.Kwakuwa eid el-haji ni eid ya kuchinja,hivyo Ng'ombe alichinjwa na nyama kugawiwa swadaka kwa jumuiya inayozunguka chuo cha St.Augustine.Pia jumuiya ya wanachuo wakiislam walishiriki na watoto yatima wa kituo cha Upendo Daima kilichopo Malimbe.Mbali ya kushiriki na watoto hao pia watoto hao walipewa vitu mbalimbali kama mafuta,sabuni,mchele na mbuzi mmoja.Vitu hivyo vilikabidhiwa na makamu mkuu wa chuo (vc)Father Charles Kitima.Jumuiya ya Waislam pia walisherehekea eid kwa kupanda miti mia moja na tatu,mitatu ikiwa ya matunda na mingine ya kawaida wakiongozwa na makamu mkuu wa chuo Dr.Kitime pamoja na mlezi mkuu wa jumuiya ya waislamu SAMUCO ndugu Altf Hirani.

No comments:

Post a Comment

Tafadhali tumia lugha nzuri na yenye staha katika kutoa maoni yako,kwani lugha chafu hazitavumiliwa,hivyo basi kuwa mstaarabu.Mwenyezi Mungu na akuongoze.Aamin!