Friday, November 11, 2011

WANAWAKE WASOMI WA KIISLAM KUFANYA KONGAMANO KUBWA KESHO.

Wanawake wa kiislam ambao ni wasomi kutoka vyuo vikuu jijini Mwanza kufanya kongamano kubwa katika ukumbi wa M3 uliopo Malimbe katika chuo kikuu cha Mt.Augustino-SAUT.Kongamano hilo litawakutanisha wasomi wanawake kutoka katika vyuo mbalimbali vya jiji la Mwanza.Mada zitakazo jadiliwa ni pamoja na Haki Ya Mwanamke Kwa Mumewe,Kupenda Ni Nini?Kwa Mtazamo wa Uislam na mengineyo yanayohusu Wanawake.Wahadhiri katika kongamano hilo ni Shekhat Zabibu kutoka Mwanza na wengine kutoka Mombasa,Kenya.Hivyo Waislam wote kinadada na kinamama mnakaribishwa sana.

No comments:

Post a Comment

Tafadhali tumia lugha nzuri na yenye staha katika kutoa maoni yako,kwani lugha chafu hazitavumiliwa,hivyo basi kuwa mstaarabu.Mwenyezi Mungu na akuongoze.Aamin!