Tuesday, November 1, 2011




Katika kongamano lililofanyika katika ukumbi wa M1 Jumapili ya tarehe 30/10 katika chuo cha Mt.Augustine(SAUT) cha jijini Mwanza.Kongamano lilikuwa maalum kwa kuwakaribisha mwaka wa kwanza,na kuwakutanisha wanafunzi wa vyuo vyote vya Mwanza. Vyuo vilivyoshiriki ni pamoja na wenyeji SAUT,CUHAS,BUTIMBA,FISHARIES,Ukiliguru,CBE,VETA na vyuo vingine jirani.Mashekh waliohudhuria kongamano hilo ni pamoja na Ust.Ilunga Kapungu(picha no2) pamoja na Ust.Hassan Kabeke(picha no3).Mashekhe wakiwaasa wasomi hao kwa ujumla kuacha kubadili tabia pindi wanapofika vyuoni na kuacha maadili ya Uislam.Kwani wengi wakifika vyuoni hawataki kujulikana kama wao ni waislam.Pia walitoa wito kwa wasomi mara wanapohimu kwenda kuzisaidia taasisi za kiislam badala ya kukaa pembeni na kulaum pindi mambo yanapokwenda kombo. Waislam pia wameaswa kuunganisha tabaka mbili zilizopo za walio na elimu ya mazingira na elimu ya dini.

No comments:

Post a Comment

Tafadhali tumia lugha nzuri na yenye staha katika kutoa maoni yako,kwani lugha chafu hazitavumiliwa,hivyo basi kuwa mstaarabu.Mwenyezi Mungu na akuongoze.Aamin!